lyrics
“Mwami wa Watombwe, Mlinzi wa Mila na Sheria”
Ehee… ehee eee!
Mwami weto, Mwana wa Batombwe,
Mlinzi wa mila, mlinzi wa ardhi,
Katiba imetamka — tunakutambua!
Mwami weto… mwanga wa jamiii ya Watombwe!
Mwami wa Watombwe, chimbuko la heshima,
Article mia mbili na saba, inasema wazi kabisa,
“Mamlaka ya jadi, ni taa ya taifa,”
Wewe ni mwongozi, uliyesimikwa na desturi zetu.
Ehee… ehee eee!
Mwami weto, Mwana wa Batombwe…
Katiba yasema, serikali haikuchagui,
Wewe wachaguliwa na damu ya mababu, na baraza la wazee.
Article mia mbili na nane, shahidi wa ukweli,
“Mwami huwekwa kwa desturi, na wala siyo kwa amri ya serikali.”
Wewe mlinzi wa ardhi ya mababu, katika udongo wa Batombwe,
Mlinda mipaka, msimamizi wa miti, mito, milima na Mali zote za Watombwe.
Utamaduni upo mikononi mwako.
Usuluhishi wa migogoro, amani ya vijiji vyetu vya Watombwe.
Wakati serikali ya wilaya inapita, wewe ni sauti yetu,
muwakilishi wa Watombwe, kwenye mabaraza ya utawala,
Mwami wa Watombwe, daraja kati ya mila na nchi,
Utaifa ndani ya mila, mila ndani ya taifa.
Twende pamoja na Mwami wetu, watoto wote wa Batombwe,
Heshima ya Mwami ni heshima ya ukoo.
Katiba imetambua, mila imethibitisha,
Mwami wetu… mwanga wa amani!
Ehee… ehee eee!
Katiba imetamka — tunakutambua!
Mwami wetu, fahari ya Batombwe!